UBALOZI WA MAREKANI WAIPONGEZA TTCL KWA KUTOA HUDUMA BORA ZA MAWASILIANO WAKATI WA UJIO NA UWEPO WA RAIS BARACK OBAMA HAPA NCHINI.

Kampuni ya simu Tanzania (TTCL) imepongezwa na Ubalozi wa Marekani  kwa huduma bora iliyotoa  wakati wa ujio wa Rais wa Marekani hapa nchini.

Akitoa shukrani hizo Kiongozi wa ujumbe kutoka  ubalozi wa Marekani  hapa nchini Bw. Jeff Shrader  amesema, Ubalozi wa Marekani Nchini Tanzania umejipatia sifa kubwa kwa huduma bora na za uhakika  kutoka TTCL wakati wote wa ujio na uwepo wa Rais wa Marekeni hapa nchini.

Ameongeza kuwa huduma walizozipata  zimethibitishwa na taarifa kutoka ofisi inayoratibu safari za Rais wa Marekani kuwa katika nchi walizopita Afrika huduma ya mawasiliano ialiyoipata Tanzania ilikuwa ni ya kiwango cha juu na aliipongeza TTCL na kusema hii ni sifa kubwa kwa Serikali ya Tanzania na Ubalozi wa Marekani hapa nchini.

Akipokea salam hizo za shukrani kutoka kwa ujumbe huo wa Marekani, Afisa Mtendaji Mkuu wa TTCL Dkt. Kamugisha Kazaura  amesema, TTCL ilifanya kazi yake kwa uhakika na ina uwezo wa kuhimili mahitaji ya watanzania na Kimataifa pia.

Ameongeza kuwa TTCL inaendelea na juhudi za kujikita zaidi katika huduma ya data/ intanet na kuendelea kuboresha gharama ili kila mtanzania apate fursa ya kunufaika na mawasiliano ya simu pamoja na data.

Katika Shukurani zake Bw. Jeff Shrader alioa pia zawadi kwa Afisa Mtendaji Mkuu wa TTCL Dkt. Kamugisha Kazaura  na kwa baadhi ya wawakilishi kutoa fani mbalimbali za Ufundi na Biashara kwa niaba ya wafanyakazi wote wa TTCL kama ishara yao ya shukurani kwa TTCL na Taifa kwa ujumla.







Comments

Popular Posts