UPATIKANAJI WA VOCHA ZA TTCL KATIKA HUDUMA ZA BENKI.
TTCL imerahisisha upatikanaji wa vocha za TTCL
kupitia huduma za kibenki kwa njia ya simu za mkononi. Mteja wa TTCL anaweza
kununua vocha moja kwa moja kupitia kwenye akaunti yake ya benki kwa
kutumia simu za mkononi.
Jumla ya benki 13 kutoa huduma ya upatikanaji
wa vocha za TTCL kwa urahisi zaidi. Benki hizo ni CRDB, Exim Bank, Dar es
salaam Community Bank, Standard Chartered Bank, Akiba Commercial Bank, Tanzania
Postal Bank, Mkombozi Bank, KCB Bank, Bank of Africa, Amana Bank, Umoja Switch,
Barclays Bank na Peoples Bank of Zanzibar.
Hivyo basi, mteja mwenye akaunti ya benki, na
ambaye anatumia simu ya mkononi ya mtandao wa Tigo,Vodacom, Airtel au
Zantel sasa anaweza kununua vocha ya TTCL wakati wowote na mahali
popote kwa njia ya simu ya mkononi.
Jinsi ya kupata vocha.
Mteja wa TTCL ili kupata huduma hii, anapaswa
kuwa amejisajili kwenye huduma ya benki kwa njia ya simu (Mobile Banking) ya
benki yake. Kisha, mteja anapaswa kutumia simu yake ya mkononi kwa kubofya
namba kwa mujibu wa benki aliyopo. kwa mfano; CRDB unabofya *150*03# kisha
fuata maelekezo.
Utaratibu wa kubofya kwa mabenki tajwa ni kama
ufuatavyo;-
Exim Bank
|
*150*11#
|
Dar Es Salaam Community Bank
|
*150*51#
|
Standard Chartered Bank
|
*150*65#
|
Akiba Commercial Bank
|
*150*10#
|
Tanzania Postal Bank
|
*150*21#
|
Mkombozi
Bank
|
*150*06#
|
KCB Bank
|
*150*22#
|
Bank of Africa
|
*150*13#
|
Amana Bank
|
*150*12#
|
Umoja
Switch
|
*150*17#
|
Barclays Bank
|
*150*20#
|
Peoples Bank of Zanzibar
|
*150*40#
|
CRDB
|
*150*03#
|
Kwa wateja wa benki 12 wanaweza kununua
vocha kwa viwango ambavyo vimeainishwa kwa vocha za TTCL kama ilivyoonyeshwa
hapa chini.
500/=
|
1000/=
|
2,000/=
|
5,000/=
|
10,000/=
|
30,000/=
|
60,000/=
|
100,000/=
|
200,000/=
|
360,000/=
|
450,000/=
|
1,000,000/=
|
Kwa wenye akaunti ya CRDB wanaweza
kununua vocha TTCL kwa kiwango chochote bila kufuata viwango hivyo hapo
juu.
Kutumia huduma hii kupitia CRDB fuata maelekezo
yafuatayo:
o Bofya *150*03#
o Chagua namba 5
o Chagua namba 5
(namba
5 inasimama badala ya TTCL. Hivyo basi, atakayechagua namba 5 atakuwa amechagua
TTCL)
o
Endelea
na maelekezo mengine
Aidha, Maxmalipo na Selcom wireless Point pia
bado wanaendelea kuuza vocha za TTCL.
Comments
Post a Comment