TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UFAFANUZI WA TAARIFA ZA MIFUMO YA KAMPUNI YA SIMU TANZANIA TTCL KUVAMIWA NA WADUKUZI.
Nicodemus Mushi,
Meneja Uhusiano TTCL
Jumanne, Februari
16, 2016, Katika Website ya Soft Pedia kulichapishwa taarifa kuwa Mifumo ya
Mawasiliano ya Kampuni ya Simu Tanzania TTCL imevamiwa na Wadukuzi na kwamba
taarifa za siri za Kampuni ya TTCL na wateja wake haziko salama.
Baada ya utafiti wa
kina na majaribio ya kitaalamu, tunapenda kuwathibithia Wateja wetu wote wa
ndani na nje ya nchi, wadau wetu na Umma kwa ujumla kwamba, taarifa hizi si
sahihi, na kwamba mifumo yetu ya Mawasiliano ya TTCL ipo salama, huduma zetu
zote zipo thabiti na mpaka sasa tunapotoa taarifa hii, hakuna uhalifu wowote
uliofanyika kwa sisi wenyewe kama Kampuni wala kwa mteja wetu yeyote.
Pamoja na taarifa
hizi, Wataalamu wetu wanaendelea kuwa
macho kwa muda wote, ili kuhakikisha kuwa, wanafanyia kazi kila taarifa ama
tishio la kiusalama linaloweza kujitokeza.
TTCL inaendelea
kuwaomba Umma na Wateja wetu wote kuendelea na majukumu yao kama kawaida bila
wasiwasi wowote. TCCL inawaleta Karibu.
Comments
Post a Comment